Mikopo ya SME Iliyohakikishwa kwa Kitabu cha Magari

Mkopo wetu wa LBF unalenga wafanyabiashara, wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi ambao watapata mkopo kulingana na mtiririko wa fedha zao huku gari la mtu likitumika kama dhamana. Kiasi cha mkopo kinaweza kuwa kati ya Tsh 2,000,000 hadi Tsh 30,000,000 kulingana na mtiririko wako wa fedha. Tutazingatia utendaji wa biashara yako au mishahara ya miezi 3. Mmoja wa maafisa wetu wa mikopo wenye uzoefu atatathmini maombi yako na mahitaji ya biashara dhidi ya hatari na kisha kukushauri ipasavyo. Bidhaa hii inapatikana katika miji mikuu ifuatayo na maeneo yake ya jirani; Dar es Salaam, Dodoma, Moshi, Arusha, na Mwanza.

Ifuatayo ni sifa na mahitaji ya mikopo ya LBF:

  1. Lazima umiliki gari.
  2. Bima inaweza kuwa ndogo au kubwa kulingana na kiasi cha mkopo
  3. Lazima uwe na Kitambulisho cha Taifa na leseni ya udereva.
  4. Barua ya utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa
  5. Taarifa ya benki ya angalau miezi 6
  6. Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi – TIN
  7. Kitambulisho cha Taifa cha mdhamini.
  8. Leseni ya Biashara/Kivuli cha Mkataba wa Ajira
  9. Picha 2 za Pasipoti
  10. Kwa mfanyakazi, lazima awe na slipu ya mshahara ya angalau miezi 3 na katika hali hii na Kivuli cha kitambulisho cha kazi.
Scroll to Top